Insha ya ajali barabarani.

Tulipofika kwenye mteremko, gari lilianza kuyumba yumba na kiacha barabara, mbele yetu Lori likija Kwa Kasi na Lo! Tuligongana. Ilikuwa siku ya ijumaa nilipodamka bukurala nikiwa nimejawa na furaha na buraha. Nilistaftahi na kugikwatua kwatukwatu tayari kuenda jijini Mombasa kufanya shughuli za kikazi.

Kazi yangu ilikuwa ya kuwanasa mapwagu na mapwaguzi jijini Nairobi. Nilikuwa mtu mashuhuri sana. Mabwanyenye Kwa watumwa walinipongeza Kwa kazi yangu njema ya kuwanasa wezi na wanyangani. Waligua hakwaa mwizi alitoka mikononi wangu. Nilifanya kazi yangu Kwa udi na uvumba Hadi wezi waliaadimika kama wali wa daku.

Niliwahi kazini kuchelewa kidogo Kwa sababu manyunyu ya mvua yalinifanya nitembee mwendo wa lumbwi. Kabla ya kubwaga roho kitini, Simu ililia. Niliiokota na kuuliza ninani aliyekuwa akinipigia.”Juma.” Sauti ya kutetemesha nchi ilinena.”Nimewaona washiriki wa genge la almasi changamwe hapa Mombasa.

Fanya Halahala ama utapata mwana si wako. Juma aliendelea. Sikungoja mwadhini aadini ili aadunasi wakaswali Bali nilifungua pijo nambari miguu na kuenda Kwa rafiki yangu. Sahibu wa udi na uvumba anisaidie na gari yake. Kwa bahati mbaya alikuwa anaitimia. Sikusuhwa moyo Bali ni upendo kwenye slani ni kapaa la daladala Hadi slani ya kuchukua magari ya kuenda Mombasa.

Nililipa nauli na nikapanda basi. Basi Hilo lilikuwa halina mtu hata mmoja ndani. Lakini baada ya muda si muda, watu walijaa Sako Kwa bako basini. Dereva aliwasha gari na tukaanza safari yetu.

Sasa nilikuwa njiani kwenye basi lile like . Dereva alianza kunywa pombe. Watu walimsihi ampe nafasi mtu mwingine, lakini alikataa Abadan kataan kumwachia. Hapo ndipo tukagongana na Lori. Watu walianza kulia kwikwikwi Kwa uchungu. Mimi nilitoka Kwa basi bila majeruhi. Watu waliuumia walipelekewa hospitalini telki mithili ya risasi.

Nilifika Mombasa salama bin salimini nilinasa genge la wezi. Kuwanasa haikuwa rahisi. Walinifyatulia risasi wakitarajia kunipeleka ahera bila nauli. Sikuogopa wala kugota. Nilijaribu Tena na Tena mpaka nikawanasa na usaidizi wa polisi wenzangu.

Similar Posts