Insha ya masimulizi Fungate ya machozi.
katika insha ya masimulizi mwandishi hutakiwa kusimulia kuhusu jambo ambalo huenda akawa alilishuhudia, aliambiwa na mtu fulani au analibuni moja kwa moja kana kwamba Liliwahi kutokea.
insha.
Kwa baadhi yetu hatujui maana ya kuwa na masikio. Wengine huyatumia kusikiliza tu huku mioyo yao ikikataa kusikiza. Kwa wengi, kuna wale hawafuati sheria au maneno tu ndogo inayoweza kuwaletea majuto au kifo.
Kwa kweli kuna wale wameponea chupuchupu na kuna wengine wamo gerezani kufungwa funguo la maisha, wengine wamefariki kutosikiliza na wengine ni majuto kwa kutofanya kitu kilichokaa.

Majuto kama hili lilifanyikia Brian. Brian Alilolewa katika jijini la zuba ambapo familia yake Ilibarikiwa na mali utajiri. Baba na mama yake wamekuwa na bidii za mchwa kufika pale wako saini na kulelea Brian kuwa awe mtoto mzuri.
Brian alisomea shule ya upili lenana na kuelekea kusomea chuo kikuu cha Havard huko marekani na kufanikiwa kupata kazi na baadae kuwa na kampuni yake Brian and Brian company. Baada ya mwaka fupi, alianza urafiki na msichana moja anayeitwa Melisa. Alikuwa msichana moja ambae alisifika na alijitunza na akawa na heshima na pia nidhamu.
Kwa miezi kadha urafiki huu ukawa umegeuka kuwa kitu kingine. Kwa vile hawa wawili walikutana kila siku kuhusu maisha yao ya kesho, na pia kufungua mioyo na kupanga mikakati za siku za usoni.
Haya yote ikampa Brian nguvu kujionyesha kuwa anaweza kuwa mume bora kwa mkewe melisa. Japo sikuwa moja, alipanga apatane na melisa katikahoteli ya Java, walikunywa kahawa na Brian alipiga magoti na kuvisha pete iliyokuwa ina metameta kama nyota.
Hayawi hayawi huwa. Harusi lilipangwa na Bwana na Bibi harusi walifunga ndoa. Hungeamini siku hilo kwa kuwa Brian alimgojea kwa hamu na ghamu kuona Melisa akiingia ndani ya kanisani kwa mwendo aste aste. Kasisi alipowavisha pete na kuwaombea, safari yao uka anza.
Brian na melisa kwa kweli walifaana, kila uchao walifurahia kama ndama. Fungate yao ilikuwa baharini mombasa ambapo waliogelea maji baridi shadidi ya chumvi, Hoteli kuu ya flamingo yalikuwa chiuma lao cha kulala. Kila walipotembea walishikana mikono wakiwa na raha yaliyoipata ilivitoa vicheko ambavyo vingefanya wenye wivu kuchemkwa na wivu.
kati ya raha huu , brian alikuwa ameyanywa chupa cha pombe mzima akiwa anona mechi za kandanda. Manchester united pinzani wao wakiwa Chelsea. Jambo lililosikitisha alikuwa amelewa na kwa masaa yao waliona wanachelewa kufika chumbani mwao.
Brian na melisa, walianza safari kurudi hoteli. Melisa alikataza Brian asiendeshe gari lakini brian alijigamba kuwa bado ana nguvu na uwezo wa kuendesha gari hilo. Brian alendesha gari hili kwa kasi sana, kwa injili ya haoy ukawa ajali.
Wote wawili Brian na Melisa walikimbizwa hospitalini kwa ambulensi. Kulikuwa na msamaria mwema aliowasaidia na kuwatoa katika ajali hilo. Brian kwa bahati aliponea chupu chupu na hakufariki. Brian alipoulizia Melisa, matokeo ilikuwa huzuni mno. Melisa matokeo ikawa kuwa ameenda kwa mola wake, kifo chake kilikuwa alishiwa damu. Machozi ya Brian yalianza kupukutika njia mbili mbili hapa Akisimama kitutwe.
Jambo hili lilimkera Brian maishani mwake na kumpa majuto. Kwa yale alifanya ilisababisha kifo cha mpenzi wake melisa. Fungate uliokuwa ya furaha na buraha ukaisha na machungu na huzuni. Anatamani sana masaa yarudi nyuma arekebishe tendo lake. kwa kweli fungate ulikuwa ya machozi.