Vitendawili sifa na aina zake.

Vitendawili ni fungu la maneno linalo na maana fiche mtu hutajika kufikiria ili maana kufumbuliwa.



Sifa za vitendawili.

– Huwa na formular maalum.(mtindo wa kwanza) – Kitendawili ………. tega.

– Husisha vifungu vinachohitaji kufunguliwa.

– Anayetegua anaposhindwa anatoa zawadi ama jibu.

– Hurejelea mambo ya kawaida katika maisha na mazingira ya wanajamii.

– Aghalabu kitendawili huwa na jibu moja tu.

– Hutumia lugha ya mkato – kauli au sentensi moja tu.

– Huchemsha bongo

– Huelimisha wanajamii.

– Hukuza stadi ya umakinifu.

– Huburudisha hadhira.

– Hukuza ufasaha wa lugha.

– Ni njia kuhifadhi utamaduni na historia ya jamii.



Aina za vitendawili.

– Vitendawili sahili (kawaida).

– Vitendawili changamano.

– Vitendawili vya sauti.

– Vitendawili mkufu.





1. Vitendawili sahili – kwa mfano: chakula kikuu cha mtoto – maziwa.

2. Vitendawili changamano – kwa mfano: amezaliwa ali, amekufa hali, amerudi hali – Nywele.

3. Vitendawili vya sauti – Chubuluu! – linapoanguka majini.

4. Vitendawili mkufu.(virefu) – Asubuhi ana miguu minne, saa saba ana miguu miwili, na jioni ana miguu mitatu. : Mtu akiwa mtoto, umri wa makamuu na akiwa mzee.

BLACK FRIDAY DEFACTO DEALS

Similar Posts